

Lugha Nyingine
2017福布斯华人富豪榜:王健林稳居亚洲首富位置
BEIJING - Kamati ya usimamizi wa mali za serikali ya China jana Jumanne imetangaza uzinduzi wa Kundi la Kampuni za Kuunda Magari za Changan kuwa kampuni ya kiviwanda inayomilikiwa na serikali kuu (SOE).
Hatua hiyo inaleta jumla ya idadi ya kampuni za kiviwanda zinazomilikiwa na serikali kuu ya China kufikia 100, na kuiweka kampuni hiyo kuwa SOE ya serikali kuu ya tatu ya nchi hiyo katika sekta ya magari, ikiungana na Kundi la Kampuni za Magari za FAW na Kampuni ya Magari ya Dongfeng.
Kampuni hiyo ina matawi 117, yenye biashara zinahusika na masuala ya magari na vipuri vya magari, pikipiki, na huduma za mambo ya fedha na uchukuzi.
Itazingatia katika kukuza nguvu mpya za uzalishaji zenye sifa bora kama vile roboti za gari za AI na ujumuishi wa AI. Inatarajiwa pia kuharakisha upanuzi wa kimataifa, ikilenga masoko kama vile Asia Kusini Mashariki, Mashariki ya Kati, Ulaya, na Amerika ya Kati na Kusini.
Wafuatiliaji wa sekta hiyo wanaona hatua hiyo ni muhimu katika juhudi pana za China za kuleta mageuzi katika SOEs za serikali kuu na kugawa mtaji wa serikali kwa njia iliyoboreshwa, wakati huohuo pia ikiimarisha uwezo wa ushindani wa kimataifa wa sekta ya magari ya nchi hiyo.
Mandhari ya Kipekee ya Karst katika Mkoa wa Guizhou yavutia watalii
Tamasha la kimataifa la densi lafunguliwa katika Mkoa wa Xinjiang, China likiwa na maonyesho 52
Wakulima wa China wawa na pilikapilika za uzalishaji wa kilimo katika kipindi cha Dashu
Maliasili nyingi za chumvi zaongeza mapato ya wanakijiji katika Wilaya ya Gegye, Xizang, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma